Isa. 17:8-13 Swahili Union Version (SUV)

8. Wala hataziangalia madhabahu, kazi ya mikono yake; wala hatavitazama vilivyofanyika kwa vidole vyake, maashera na sanamu za jua.

9. Katika siku hiyo miji yake yenye maboma itakuwa kama mahali palipoachwa ndani ya mwitu, na juu ya kilele cha mlima, palipoachwa mbele ya wana wa Israeli; napo patakuwa ganjo.

10. Maana umemsahau Mungu wa wokovu wako, wala hukuukumbuka mwamba wa ngome yako; kwa sababu hiyo ulipanda mashamba yapendezayo, na kutia ndani yake mizabibu migeni.

11. Katika siku ile ulipopanda, ulifanya kitalu, na wakati wa asubuhi ulizimeesha mbegu zako, lakini mavuno yatatoweka siku ya huzuni, na ya sikitiko la moyo lifishalo.

12. Aha! Uvumi wa watu wengi!Wanavuma kama uvumi wa bahari;Aha! Ngurumo ya mataifa!Wananguruma kama ngurumo ya maji mengi;

13. Mataifa wananguruma kama ngurumo ya maji mengi;Lakini atawakemea, nao watakimbia mbali sana,Watafukuzwa kama makapi milimani mbele ya upepo,Na kama mavumbi vuruvuru mbele ya tufani.

Isa. 17