1. Sala ya nabii Habakuki.
2. Ee BWANA, nimesikia habari zako, nami naogopa;Ee BWANA, fufua kazi yako katikati ya miaka;Katikati ya miaka tangaza habari yake;Katika ghadhabu kumbuka rehema.
3. Mungu alikuja kutoka Temani,Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani.Utukufu wake ukazifunika mbingu,Nayo dunia ikajaa sifa yake.
4. Mwangaza wake ulikuwa kama nuru;Alikuwa na mishale ya nuru ubavuni pake;Ndipo ulipofichwa uweza wake.
5. Mbele zake ilikwenda tauni,Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake.
6. Akasimama, akaitetemesha dunia;Akatazama, akawasitusha mataifa;Na milima ya zamani ikatawanyika;Vilima vya kale vikainama;Miendo yake ilikuwa kama siku za kale.
7. Naliziona hema za Kushani katika taabu;Mapazia ya nchi ya Midiani yakatetemeka.
8. Je! BWANA aliikasirikia mito?Je! Hasira yako ilikuwa juu ya mito,Au ghadhabu yako juu ya bahari,Hata ukapanda farasi zako,Katika magari yako ya wokovu?
9. Uta wako ukafanywa wazi kabisa;Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti;Ukaipasua nchi kwa mito.