Hab. 3:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Sala ya nabii Habakuki.

2. Ee BWANA, nimesikia habari zako, nami naogopa;Ee BWANA, fufua kazi yako katikati ya miaka;Katikati ya miaka tangaza habari yake;Katika ghadhabu kumbuka rehema.

3. Mungu alikuja kutoka Temani,Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani.Utukufu wake ukazifunika mbingu,Nayo dunia ikajaa sifa yake.

4. Mwangaza wake ulikuwa kama nuru;Alikuwa na mishale ya nuru ubavuni pake;Ndipo ulipofichwa uweza wake.

5. Mbele zake ilikwenda tauni,Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake.

6. Akasimama, akaitetemesha dunia;Akatazama, akawasitusha mataifa;Na milima ya zamani ikatawanyika;Vilima vya kale vikainama;Miendo yake ilikuwa kama siku za kale.

7. Naliziona hema za Kushani katika taabu;Mapazia ya nchi ya Midiani yakatetemeka.

8. Je! BWANA aliikasirikia mito?Je! Hasira yako ilikuwa juu ya mito,Au ghadhabu yako juu ya bahari,Hata ukapanda farasi zako,Katika magari yako ya wokovu?

Hab. 3