10. Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya IsraeliBaada ya siku zile, asema Bwana;Nitawapa sheria zangu katika nia zao,Na katika mioyo yao nitaziandika;Nami nitakuwa Mungu kwao,Nao watakuwa watu wangu.
11. Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake,Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana;Kwa maana wote watanijua,Tangu mdogo wao hata mkubwa wao.
12. Kwa sababu nitawasamehe maovu yao,Na dhambi zao sitazikumbuka tena.
13. Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka.