Ayu. 12:1-8 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,

2. Hapana shaka ninyi ndinyi watu halisi,Nanyi mtakapokufa, ndipo na hekima itakoma.

3. Lakini mimi pia, nina fahamu kama ninyi;Mimi si duni yenu ninyi;Naam, ni nani asiyejua mambo kama hayo?

4. Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake,Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu;Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko.

5. Katika mawazo yake huyo aliye na raha mna kudharau mashaka;Tayari kwa ajili ya wenye kuteleza miguu.

6. Hema za wapokonyi hufanikiwa,Na hao wamkasirishao Mungu hukaa salama;Mikononi mwao Mungu huleta vitu vingi.

7. Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha;Na nyuni wa angani, nao watakuambia;

8. Au nena na nchi, nayo itakufundisha;Nao samaki wa baharini watakutangazia.

Ayu. 12