Amu. 5:18-26 Swahili Union Version (SUV)

18. Zabuloni ndio watu waliohatirisha roho zao hata kufa;Nao Naftali mahali palipoinuka kondeni.

19. Wafalme walikuja wakafanya vita,Ndipo wafalme wa Kanaani walifanya vita.Katika Taanaki, karibu na maji ya Megido;Hawakupata faida yo yote ya fedha.

20. Walipigana kutoka mbinguni,Nyota katika miendo yao zilipigana na Sisera.

21. Mto ule wa Kishoni uliwachukua,Ule mto wa zamani, mto wa Kishoni.Ee roho yangu, endelea mbele kwa nguvu.

22. Ndipo kwato za farasi zilikanyaga-kanyagaKwa sababu ya kupara-para,Kupara-para kwao wenye nguvu.

23. Ulaanini Merozi, alisema malaika wa BWANA,Walaanini kwa uchungu wenyeji wake;Kwa maana hawakuja kumsaidia BWANA,Kumsaidia BWANA juu ya hao wenye nguvu.

24. Atabarikiwa Yaeli kuliko wanawake wote;Mkewe Heberi, Mkeni,Atabarikiwa kuliko wanawake wote hemani.

25. Aliomba maji, naye akampa maziwa.Akamletea siagi katika sahani ya heshima.

26. Akanyosha mkono wake akashika kigingi,Nao mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi;Akampiga Sisera kwa hiyo nyundo, akamtoboa kichwa chake.Naam, alimpiga akamtoboa kipaji chake.

Amu. 5