Amu. 5:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Ndipo Debora, na Baraka mwana wa Abinoamu, wakaimba siku ile, wakisema;

2. Kwa sababu wakuu walitangulia katika Israeli,Kwa sababu watu walijitoa nafsi zao kwa hiari yao,Mhimidini BWANA.

3. Sikieni, enyi wafalme; tegeni masikio, enyi wakuu;Mimi, naam mimi, nitamwimbia BWANA;Nitamhimidi BWANA, Mungu wa Israeli.

4. BWANA, ulipotoka katika Seiri,Ulipokwenda vitani kutoka mashamba ya Edomu,Nchi ilitetema, mbingu nazo zikadondoza maji,Naam, mawingu yakadondoza maji.

5. Milima ikayeyuka mbele za uso wa BWANA,Naam hata Sinai ule mbele za uso wa BWANA, Mungu wa Israeli.

6. Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi,Siku za Yaeli, njia kuu zilikuwa hazina watu;Nao wenye kusafiri walipita kwa njia za kando.

Amu. 5