1 Nya. 21:5-11 Swahili Union Version (SUV)

5. Naye Yoabu akamtolea Daudi jumla ya hesabu ya watu. Na hao wote wa Israeli walikuwa watu elfu mara elfu, na mia elfu, wenye kufuta panga; na wa Yuda watu mia nne na sabini elfu, wenye kufuta panga.

6. Lakini Lawi na Benyamini hakuwahesabu miongoni mwao; kwa sababu neno la mfalme limemchukiza Yoabu.

7. Neno hilo likawa baya machoni pa Mungu; kwa hiyo akawapiga Israeli.

8. Naye Daudi akamwambia Mungu, Nimekosa sana, kwa kuwa nimelifanya jambo hili; lakini sasa uuondolee mbali, nakusihi, uovu wa mtumwa wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa.

9. Naye BWANA akanena na Gadi, mwonaji wake Daudi, akisema,

10. Nenda ukanene na Daudi, ukisema, BWANA asema hivi, Nakuwekea mambo matatu; katika haya ujichagulie moja, nikutendee hilo.

11. Basi Gadi akamwendea Daudi, akamwambia, BWANA asema hivi, Kubali upendavyo;

1 Nya. 21