1 Fal. 15:5-7 Swahili Union Version (SUV)

5. kwa sababu Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa BWANA, wala hakukosa katika yote aliyomwamuru, siku zote za maisha yake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.

6. Basi kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote za maisha yake.

7. Na mambo yote ya Abiya yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.

1 Fal. 15