Yeremia 10:16-20 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Lakini Mungu wa Yakobo si kama vinyago hivyo,maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote,na Israeli ni taifa lililo mali yake;Mwenyezi-Mungu wa majeshi ndilo jina lake.

17. Kusanyeni vitu vyenu enyi watu mliozingirwa.

18. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wakati huo nitawatupa nje ya nchi hii,nitawataabisha asibaki mtu yeyote.”

19. Ole wangu mimi Yerusalemu maana nimejeruhiwa!Jeraha langu ni baya sana!Lakini nilisema: “Hakika haya ni mateso,na sina budi kuyavumilia.”

20. Lakini hema langu limebomolewa,kamba zake zote zimekatika;watoto wangu wameniacha, na kwenda zao,wala hawapo tena;hakuna wa kunisimikia tena hema langu,wala wa kunitundikia mapazia yangu.

Yeremia 10