Isaya 59:4-7 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Hakuna atoaye madai yake kwa haki,wala anayeshtaki kwa uaminifu.Mnategemea hoja batili;mnasema uongo.Mnatunga hila na kuzaa uovu.

5. Mnaangua mayai ya joka lenye sumu,mnafuma utando wa buibui.Anayekula mayai yenu hufa,na yakipasuliwa nyoka hutokea.

6. Utando wenu haufai kwa mavazi,watu hawawezi kujifunikia mnachofuma.Kazi zenu ni kazi za uovu,matendo yenu yote ni ukatili mtupu.

7. Mko mbioni kutenda maovu,mnaharakisha kumwaga damu isiyo na hatia.Mawazo yenu ni mawazo ya uovu,popote mwendapo mnaacha ukiwa na uharibifu.

Isaya 59