Isaya 43:21-25 Biblia Habari Njema (BHN)

21. watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe,ili wazitangaze sifa zangu!’

22. “Lakini ewe taifa la Yakobo, hukuniabudu mimi;enyi watu wa Israeli, mlinichoka mimi!

23. Hamjaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa,wala kuniheshimu kwa tambiko zenu.Nami sikuwalemeza kwa kutaka sadaka,wala sikuwachosha kwa kuwadai ubani.

24. Hamkuninunulia manukato kwa faida yenu,wala kuniridhisha kwa nyama nono za tambiko.Badala yake dhambi zenu zimekuwa mzigo kwangu,mmenichosha kabisa kwa makosa yenu.

25. Walakini mimi ndimi niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu,ndimi niyafutaye makosa kwa ajili yangu mwenyewe,na wala sitazikumbuka dhambi zenu.

Isaya 43