Zab. 95:7-10 Swahili Union Version (SUV)

7. Kwa maana ndiye Mungu wetu,Na sisi tu watu wa malisho yake,Na kondoo za mkono wake.Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!

8. Msifanye migumu mioyo yenu;Kama vile huko MeribaKama siku ya Masa jangwani.

9. Hapo waliponijaribu baba zenu,Wakanipima, wakayaona matendo yangu.

10. Miaka arobaini nalihuzunika na kizazi kile,Nikasema, Hao ni watu waliopotoka mioyo,Hawakuzijua njia zangu.

Zab. 95