7. Kwa maana ndiye Mungu wetu,Na sisi tu watu wa malisho yake,Na kondoo za mkono wake.Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
8. Msifanye migumu mioyo yenu;Kama vile huko MeribaKama siku ya Masa jangwani.
9. Hapo waliponijaribu baba zenu,Wakanipima, wakayaona matendo yangu.
10. Miaka arobaini nalihuzunika na kizazi kile,Nikasema, Hao ni watu waliopotoka mioyo,Hawakuzijua njia zangu.