Zab. 95:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Njoni, tumwimbie BWANA,Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.

2. Tuje mbele zake kwa shukrani,Tumfanyie shangwe kwa zaburi.

3. Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu,Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.

4. Mkononi mwake zimo bonde za dunia,Hata vilele vya milima ni vyake.

5. Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya,Na mikono yake iliumba nchi kavu.

Zab. 95