4. Heri wakaao nyumbani mwako,Wanakuhimidi daima.
5. Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako,Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake.
6. Wakipita kati ya bonde la Vilio,Hulifanya kuwa chemchemi,Naam, mvua ya vuli hulivika baraka
7. Huendelea toka nguvu hata nguvu,Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu.
8. BWANA, Mungu wa majeshi, uyasikie maombi yangu,Ee Mungu wa Yakobo, usikilize,
9. Ee Mungu, ngao yetu, uangalie,Umtazame uso masihi wako.
10. Hakika siku moja katika nyua zakoNi bora kuliko siku elfu.Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu,Kuliko kukaa katika hema za uovu.