Zab. 80:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Wewe uchungaye Israeli, usikie,Wewe umwongozaye Yusufu kama kundi;Wewe uketiye juu ya makerubi, utoe nuru.

2. Mbele ya Efraimu, na Benyamini, na Manase,Uziamshe nguvu zako,Uje, utuokoe.

3. Ee Mungu, uturudishe,Uangazishe uso wako nasi tutaokoka.

4. Ee BWANA, Mungu wa majeshi, hata liniUtayaghadhibikia maombi ya watu wako?

5. Umewalisha mkate wa machozi,Umewanywesha machozi kwa kipimo kikuu.

Zab. 80