Zab. 78:9-13 Swahili Union Version (SUV)

9. Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde,Walirudi nyuma siku ya vita.

10. Hawakulishika agano la Mungu;Wakakataa kuenenda katika sheria yake;

11. Wakayasahau matendo yake,Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.

12. Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu,Katika nchi ya Misri, konde la Soani.

13. Aliipasua bahari akawavusha;Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.

Zab. 78