Zab. 78:65-69 Swahili Union Version (SUV)

65. Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi,Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo;

66. Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma,Akawatia aibu ya milele.

67. Ila akaikataa hema ya Yusufu;Wala hakuichagua kabila ya Efraimu.

68. Bali aliichagua kabila ya Yuda,Mlima Sayuni alioupenda.

69. Akajenga patakatifu pake kama vilele,Kama dunia aliyoiweka imara milele.

Zab. 78