Zab. 78:58-63 Swahili Union Version (SUV)

58. Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,Wakamtia wivu kwa sanamu zao.

59. Mungu akasikia, akaghadhibika,Akamkataa Israeli kabisa.

60. Akaiacha maskani ya Shilo,Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;

61. Akaziacha nguvu zake kutekwa,Na fahari yake mkononi mwa mtesi.

62. Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga;Akaughadhibikia urithi wake.

63. Moto ukawala vijana wao,Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

Zab. 78