55. Akawafukuza mataifa mbele yao,Akawapimia urithi kwa kamba,Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao.
56. Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi,Wala hawakuzishika shuhuda zake.
57. Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao;Wakaepea kama upinde usiofaa.
58. Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
59. Mungu akasikia, akaghadhibika,Akamkataa Israeli kabisa.
60. Akaiacha maskani ya Shilo,Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
61. Akaziacha nguvu zake kutekwa,Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
62. Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga;Akaughadhibikia urithi wake.