28. Akawaangusha kati ya matuo yao,Pande zote za maskani zao.
29. Wakala wakashiba sana;Maana aliwaletea walivyovitamani;
30. Hawakuachana na matakwa yao.Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao
31. Hasira ya Mungu ikapanda juu yao,Akawaua waliokuwa wanono;Akawaangusha chini vijana wa Israeli.
32. Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi,Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.