23. Lakini aliyaamuru mawingu juu;Akaifungua milango ya mbinguni;
24. Akawanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.
25. Mwanadamu akala chakula cha mashujaa;Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
26. Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni;Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
27. Akawanyeshea nyama kama mavumbi,Na ndege wenye mbawa,Kama mchanga wa bahari.
28. Akawaangusha kati ya matuo yao,Pande zote za maskani zao.