21. Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika;Moto ukawashwa juu ya Yakobo,Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
22. Kwa kuwa hawakumwamini Mungu,Wala hawakuutumainia wokovu wake.
23. Lakini aliyaamuru mawingu juu;Akaifungua milango ya mbinguni;
24. Akawanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.
25. Mwanadamu akala chakula cha mashujaa;Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
26. Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni;Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
27. Akawanyeshea nyama kama mavumbi,Na ndege wenye mbawa,Kama mchanga wa bahari.
28. Akawaangusha kati ya matuo yao,Pande zote za maskani zao.
29. Wakala wakashiba sana;Maana aliwaletea walivyovitamani;
30. Hawakuachana na matakwa yao.Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao