Zab. 78:18-25 Swahili Union Version (SUV)

18. Wakamjaribu Mungu mioyoni mwaoKwa kutaka chakula kwa tamaa zao.

19. Naam, walimwamba Mungu, wakasema,Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?

20. Tazama, aliupiga mwamba;Maji yakabubujika, ikafurika mito.Pia aweza kutupa chakula?Atawaandalia watu wake nyama?

21. Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika;Moto ukawashwa juu ya Yakobo,Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.

22. Kwa kuwa hawakumwamini Mungu,Wala hawakuutumainia wokovu wake.

23. Lakini aliyaamuru mawingu juu;Akaifungua milango ya mbinguni;

24. Akawanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.

25. Mwanadamu akala chakula cha mashujaa;Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.

Zab. 78