13. Aliipasua bahari akawavusha;Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.
14. Akawaongoza kwa wingu mchana,Na usiku kucha kwa nuru ya moto.
15. Akapasua miamba jangwani;Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.
16. Akatokeza na vijito gengeni,Akatelemsha maji kama mito.
17. Lakini wakazidi kumtenda dhambi,Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.
18. Wakamjaribu Mungu mioyoni mwaoKwa kutaka chakula kwa tamaa zao.
19. Naam, walimwamba Mungu, wakasema,Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?
20. Tazama, aliupiga mwamba;Maji yakabubujika, ikafurika mito.Pia aweza kutupa chakula?Atawaandalia watu wake nyama?
21. Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika;Moto ukawashwa juu ya Yakobo,Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
22. Kwa kuwa hawakumwamini Mungu,Wala hawakuutumainia wokovu wake.
23. Lakini aliyaamuru mawingu juu;Akaifungua milango ya mbinguni;
24. Akawanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.
25. Mwanadamu akala chakula cha mashujaa;Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
26. Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni;Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
27. Akawanyeshea nyama kama mavumbi,Na ndege wenye mbawa,Kama mchanga wa bahari.
28. Akawaangusha kati ya matuo yao,Pande zote za maskani zao.
29. Wakala wakashiba sana;Maana aliwaletea walivyovitamani;