9. Mungu amesahau fadhili zake?Amezuia kwa hasira rehema zake?
10. Nikasema, Ndio udhaifu wangu huo;Lakini nitaikumbuka miaka ya mkono wa kuume wake Aliye juu.
11. Nitayakumbuka matendo ya BWANA;Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.
12. Pia nitaitafakari kazi yako yote;Nitaziwaza habari za matendo yako.
13. Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu;Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu?