Zab. 77:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike;Naliona mashaka nisiweze kunena.

5. Nalifikiri habari za siku za kale,Miaka ya zamani zilizopita.

6. Nakumbuka wimbo wangu usiku,Nawaza moyoni mwangu,Roho yangu ikatafuta.

7. Je! Bwana atatupa milele na milele?Hatatenda fadhili tena kabisa?

8. Rehema zake zimekoma hata milele?Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?

Zab. 77