1. Nimpazie Mungu sauti yangu,Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia.
2. Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana;Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea;Nafsi yangu ilikataa kufarijika.
3. Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika;Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.
4. Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike;Naliona mashaka nisiweze kunena.