Zab. 75:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee Mungu, twakushukuru.Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu;Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.

2. Nitakapoufikia wakati ulioamriwa,Mimi nitahukumu hukumu za haki.

3. Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki,Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.

4. Naliwaambia waliojivuna, Msijivune;Na wasio haki, Msiiinue pembe.

Zab. 75