1. Ee Mungu, twakushukuru.Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu;Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.
2. Nitakapoufikia wakati ulioamriwa,Mimi nitahukumu hukumu za haki.
3. Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki,Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.
4. Naliwaambia waliojivuna, Msijivune;Na wasio haki, Msiiinue pembe.