13. Atamhurumia aliye dhaifu na maskini,Na nafsi za wahitaji ataziokoa.
14. Atawakomboa nafsi zao na kuonewa na udhalimu,Na damu yao ina thamani machoni pake.
15. Basi na aishi;Na wampe dhahabu ya Sheba;Na wamwombee daima;Na kumbariki mchana kutwa.
16. Na uwepo wingi wa nafakaKatika ardhi juu ya milima;Matunda yake na yawaye-waye kama Lebanoni,Na watu wa mjini wasitawi kama majani ya nchi.
17. Jina lake na lidumu milele,Pindi ling’aapo jua jina lake liwe na wazao;Mataifa yote na wajibariki katika yeye,Na kumwita heri.
18. Na ahimidiwe BWANA, Mungu, Mungu wa Israeli,Atendaye miujiza Yeye peke yake;
19. Jina lake tukufu na lihimidiwe milele;Dunia yote na ijae utukufu wake. Amina na Amina.
20. Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamekwisha.