Zab. 66:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Mpigie Mungu kelele za shangwe, nchi yote,

2. Imbeni utukufu wa jina lake,Tukuzeni sifa zake.

3. Mwambieni Mungu, Matendo yako yatisha kama nini!Kwa ajili ya wingi wa nguvu zako,Adui zako watakuja kunyenyekea mbele zako.

4. Nchi yote itakusujudia na kukuimbia,Naam, italiimbia jina lako.

Zab. 66