1. Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza,Mchana kutwa ananionea akileta vita.
2. Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa,Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.
3. Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;
4. Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake.Nimemtumaini Mungu, sitaogopa;Mwenye mwili atanitenda nini?