Zab. 55:20-22 Swahili Union Version (SUV)

20. Amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye,Amelihalifu agano lake.

21. Kinywa chake ni laini kuliko siagi,Bali moyo wake ni vita.Maneno yake ni mororo kuliko mafuta,Bali hayo ni panga wazi.

22. Umtwike BWANA mzigo wako naye atakutegemeza,Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.

Zab. 55