Zab. 40:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Akatia wimbo mpya kinywani mwangu,Ndio sifa zake Mungu wetu.Wengi wataona na kuogopa,Nao watamtumaini BWANA

4. Heri aliyemfanya BWANA kuwa tumaini lake,Wala hakuwaelekea wenye kiburi,Wala hao wanaogeukia uongo.

5. Ee BWANA, Mungu wangu, umefanya kwa wingiMiujiza yako na mawazo yako kwetu;Hakuna awezaye kufananishwa nawe;Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri,Ni mengi sana hayahesabiki.

6. Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,Masikio yangu umeyazibua,Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.

Zab. 40