7. Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso,Utanizungusha nyimbo za wokovu.
8. Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;Nitakushauri, jicho langu likikutazama.
9. Msiwe kama farasi wala nyumbu,Walio hawana akili.Kwa matandiko ya lijamu na hatamuSharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia.
10. Naye mtu mwovu ana mapigo mengi,Bali amtumainiye BWANA fadhili zitamzunguka.