6. Kwa hiyo kila mtu mtauwaAkuombe wakati unapopatikana.Hakika maji makuu yafurikapo,Hayatamfikia yeye.
7. Ndiwe sitara yangu, utanihifadhi na mateso,Utanizungusha nyimbo za wokovu.
8. Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;Nitakushauri, jicho langu likikutazama.
9. Msiwe kama farasi wala nyumbu,Walio hawana akili.Kwa matandiko ya lijamu na hatamuSharti kuwazuia hao, au hawatakukaribia.