5. Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo,Katika radhi yake mna uhai.Huenda kilio huja kukaa usiku,Lakini asubuhi huwa furaha.
6. Nami nilipofanikiwa nalisema,Sitaondoshwa milele.
7. BWANA, kwa radhi yakoWewe uliuimarisha mlima wangu.Uliuficha uso wako,Nami nikafadhaika.
8. Ee BWANA, nalikulilia Wewe,Naam, kwa BWANA naliomba dua.
9. Mna faida gani katika damu yanguNishukapo shimoni?Mavumbi yatakusifu?Yataitangaza kweli yako?
10. Ee BWANA, usikie, unirehemu,BWANA, uwe msaidizi wangu.
11. Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;Ulinivua gunia, ukanivika furaha.