Zab. 22:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Mungu wangu, Mungu wangu,Mbona umeniacha?Mbona U mbali na wokovu wangu,Na maneno ya kuugua kwangu?

2. Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibuNa wakati wa usiku lakini sipati raha.

3. Na Wewe U Mtakatifu,Uketiye juu ya sifa za Israeli.

4. Baba zetu walikutumaini Wewe,Walitumaini, na Wewe ukawaokoa.

5. Walikulilia Wewe wakaokoka,Walikutumaini wasiaibike.

Zab. 22