Zab. 18:29-37 Swahili Union Version (SUV)

29. Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi,Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.

30. Mungu, njia yake ni kamilifu,Ahadi ya BWANA imehakikishwa,Yeye ndiye ngao yao.Wote wanaomkimbilia.

31. Maana ni nani aliye Mungu ila BWANA?Ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu?

32. Mungu ndiye anifungaye mshipi wa nguvu,Naye anaifanya kamilifu njia yangu.

33. Miguu yangu anaifanya kuwa ya kulungu,Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

34. Ananifundisha mikono yangu vita,Mikono yangu ikaupinda upinde wa shaba.

35. Nawe umenipa ngao ya wokovu wako,Mkono wako wa kuume umenitegemeza,Na unyenyekevu wako umenikuza.

36. Umezifanyizia nafasi hatua zangu,Na miguu yangu haikuteleza.

37. Nitawafuatia adui zangu na kuwapata,Wala sitarudi nyuma hata wakomeshwe.

Zab. 18