Zab. 18:20-24 Swahili Union Version (SUV)

20. BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu,Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.

21. Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.

22. Hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu,Wala amri zake sikujiepusha nazo.

23. Nami nalikuwa mkamilifu mbele zake,Nikajilinda na uovu wangu.

24. Mradi BWANA amenilipa sawasawa na haki yangu,Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.

Zab. 18