Zab. 150:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Haleluya.Msifuni Mungu katika patakatifu pake;Msifuni katika anga la uweza wake.

2. Msifuni kwa matendo yake makuu;Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3. Msifuni kwa mvumo wa baragumu;Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4. Msifuni kwa matari na kucheza;Msifuni kwa zeze na filimbi;

5. Msifuni kwa matoazi yaliayo;Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

Zab. 150