3. BWANA ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana,Wala ukuu wake hautambulikani.
4. Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako,Kitayatangaza matendo yako makuu.
5. Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako,Na matendo yako yote ya ajabu.
6. Watu watayataja matendo yako ya kutisha,Nami nitausimulia ukuu wako.
7. Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu.Wataiimba haki yako.
8. BWANA ana fadhili, ni mwingi wa huruma,Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
9. BWANA ni mwema kwa watu wote,Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.