Zab. 141:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, nimekuita, unijie hima,Uisikie sauti yangu nikuitapo.

2. Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba,Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.

3. Ee BWANA, uweke mlinzi kinywani pangu,Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.

4. Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya,Nisiyazoelee matendo yasiyofaa,Pamoja na watu watendao maovu;Wala nisile vyakula vyao vya anasa.

Zab. 141