Zab. 139:1-9 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, umenichunguza na kunijua.

2. Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;Umelifahamu wazo langu tokea mbali.

3. Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu,Umeelewa na njia zangu zote.

4. Maana hamna neno ulimini mwanguUsilolijua kabisa, BWANA.

5. Umenizingira nyuma na mbele,Ukaniwekea mkono wako.

6. Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi,Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.

7. Niende wapi nijiepushe na roho yako?Niende wapi niukimbie uso wako?

8. Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko;Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko.

9. Ningezitwaa mbawa za asubuhi,Na kukaa pande za mwisho za bahari;

Zab. 139