1. Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2. Katika miti iliyo katikati yakeTulivitundika vinubi vyetu.
3. Maana huko waliotuchukua matekaWalitaka tuwaimbie;Na waliotuonea walitaka furaha;Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4. Tuuimbeje wimbo wa BWANAKatika nchi ya ugeni?
5. Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe,Mkono wangu wa kuume na usahau.