Zab. 137:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.

2. Katika miti iliyo katikati yakeTulivitundika vinubi vyetu.

3. Maana huko waliotuchukua matekaWalitaka tuwaimbie;Na waliotuonea walitaka furaha;Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.

4. Tuuimbeje wimbo wa BWANAKatika nchi ya ugeni?

5. Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe,Mkono wangu wa kuume na usahau.

Zab. 137