Zab. 132:4-9 Swahili Union Version (SUV)

4. Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi,Wala kope zangu kusinzia;

5. Hata nitakapompatia BWANA mahali,Na Shujaa wa Yakobo maskani.

6. Tazama, tulisikia habari zake katika Efrata,Katika konde la Yearimu tuliiona.

7. Na tuingie katika maskani yake,Tusujudu penye kiti cha kuwekea miguu yake.

8. Ee BWANA, uinuke, uende kwenye raha yako,Wewe na sanduku la nguvu zako.

9. Makuhani wako na wavikwe haki,Watauwa wako na washangilie.

Zab. 132