Zab. 132:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. BWANA, umkumbukie DaudiTaabu zake zote alizotaabika.

2. Ndiye aliyemwapia BWANA,Akaweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo.

3. Sitaingia hemani mwa nyumba yangu,Wala sitapanda matandiko ya kitanda changu;

4. Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi,Wala kope zangu kusinzia;

5. Hata nitakapompatia BWANA mahali,Na Shujaa wa Yakobo maskani.

Zab. 132