Zab. 121:2-7 Swahili Union Version (SUV)

2. Msaada wangu u katika BWANA,Aliyezifanya mbingu na nchi.

3. Asiuache mguu wako usogezwe;Asisinzie akulindaye;

4. Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5. BWANA ndiye mlinzi wako;BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6. Jua halitakupiga mchana,Wala mwezi wakati wa usiku.

7. BWANA atakulinda na mabaya yote,Atakulinda nafsi yako.

Zab. 121