1. Nitayainua macho yangu niitazame milima,Msaada wangu utatoka wapi?
2. Msaada wangu u katika BWANA,Aliyezifanya mbingu na nchi.
3. Asiuache mguu wako usogezwe;Asisinzie akulindaye;
4. Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,Yeye aliye mlinzi wa Israeli.