1. Ee nafsi yangu, umhimidi BWANA.Wewe, BWANA, Mungu wangu,Umejifanya mkuu sana;Umejivika heshima na adhama.
2. Umejivika nuru kama vazi;Umezitandika mbingu kama pazia;
3. Na kuziweka nguzo za orofa zake majini.Huyafanya mawingu kuwa gari lake,Na kwenda juu ya mabawa ya upepo,
4. Huwafanya malaika zake kuwa pepo,Na watumishi wake kuwa moto wa miali.
5. Uliiweka nchi juu ya misingi yake,Isitikisike milele.